Ugonjwa Wa Kisonono (Gonorrhoea): Chanzo Na Tiba
Ugonjwa wa Kisonono (Gonorrhoea) ni ugonjwa unaoshambulia watu wengi, wanaume kwa wanawake. Ni ugonjwa unaotibika ingawa kwa miaka ya karibuni, wadudu wa ugonjwa huu wameonyesha kuanza kutosikia tiba zinazotolewa. Kisonono
kisipotibiwa kikamilifu, huweza kuleta madhara ya kudumu kwenye mwili wa
mgonjwa na kumfanya aweze kuambukizwa au kuambukiza UKIMWI kwa urahisi.
Katika ukurasa huu tutaona chanzo cha ugonjwa huu, dalili zake na mwisho kinga
na tiba inayoweza kutolewa kwa ugonjwa huu.
Chanzo
Cha Kisonono (Gonorrhoea)
Kisonono ni ugonjwa unaoambukiza kwa ngono – sexually
transmitted infection (STI) – na unasababishwa na bakteria
aitwaye Neisseria gonorrhoeae au gonococcus. Bakteria huyu hupenda kuzaliana
kwenye maeneo ya joto, yenye unyevunyevu yakiwemo maeneo ya shingo ya uzazi
(cervix), nyumba ya uzazi (uterus), mirija ya uzazi (fallopian tubes) na mrija
wa kutolea mkojo nje (urethra). Bakteria hawa pia huweza kuzaliana kwenye
mdomo, mkundu na mara chache kwenye koo na macho.
Kimsingi bakteria hawa hupatikana kwa wingi katika shahawa na
usaha unaotoka katika uume wa mwanamme mgonjwa na katika majimaji ya ukeni.
Bakteria hawa huambukiza kutoka mtu mmoja hadi mwingine kwa njia zifuatazo:
Ngono zembe kupitia uke, mdomo au mkundu. Mwanamme anaweza
kumwambukiza gono mwanamke hata kama hakutoa shahawa (manii) wakati wa kufanya
tendo la ndoa
Kuchangia vifaa vya kujistarehesha ambavyo havikuoshwa au kufunikwa na kondomu, kama vibrators na vimwanasesere
vya aina nyingine.
Kuchangia vifaa vya kujistarehesha ambavyo havikuoshwa au kufunikwa na kondomu, kama vibrators na vimwanasesere
vya aina nyingine.
Mama mjamzito mwenye maambukizi anaweza kumwambukiza mtoto
anayezaliwa na endapo mtoto huyo hatapewa tiba, anaweza
kupata upofu wa kudumu. Hivyo, mama mjamzito mwenye maambukizi anatakiwa apewe tiba kabla ya kujifungua.
kupata upofu wa kudumu. Hivyo, mama mjamzito mwenye maambukizi anatakiwa apewe tiba kabla ya kujifungua.
Bakteria wa kisonono hawaambukizi kwa kubusiana, kushikana
mikono, kuchangia bafu au taulo, mabwawa ya kuogelea, vyoo, kuchangia vikombe
na vyombo ya kulia kwa sababu wadudu hawa wa kisonono hawana uwezo wa kuishi
kwa muda mrefu nje ya mwili wa binadamu.
Dali Za
Kisonono
Sio watu wote wenye kisonono wataona dalili za ugonjwa huu. Pale
ambapo mgonjwa ataona dalili, zitaonekana katika siku kama 10 baada ya kupata
maambukizi ingawa inaweza ikachukua hadi siku 30. Dalili atakazoziona mwanamme
zinaweza kuwa tofauti kidogo na zile atakazoziona mwanamke.
Dalili Za Kisonono Kwa Mwanaume
Kutokwa na uchafu uumeni wenye rangi
nyeupe, njano au kijani unaofanana na usaha Maumivu kwenye mapumbu.Maumivu wakati wa haja ndogo Kutokwa na uchafu kwenye mkundu, kuwashwa, kutokwa damu
wakati wa haja kubwa.Koo kukauka, kuwashwa, kumeza kwa shida au uvimbe shingoni. Maumivu kwenye macho, macho kutopenda mwanga mwingi na
kutokwa uchafu machoni unafanana na usaha .Maumivu na kuvimba kwenye sehemu za maungio ya mifupa
Dalili
Za Kisonono Kwa Mwanamke
Kisonono
kinaweza kumsababishia mwanamke kuzaa njiti (mtoto kuzaliwa kabla ya siku) au
mimba kuharibika. Mwanamke mwenye kisonono anaweza kumwambukiza kichanga wakati
wa uzazi na kukisababishia kichanga upofu wa kudumu, maambukizi kwenye maungio
ya mifupa au maambukizi kwenye damu.
Mwanamme ambaye
ana kisonono isiyotibiwa anaweza kupata maumivu makali kwenye mapumbu kutokana
na ugonjwa uitwao
epididymo- orchitis na kumsababishia ugumba. Kisonono ambayo haikupewa tiba ya kutosha inaweza kumletea madhara kwenye tezi dume (prostate) na anaweza kupata makovu ndani ya mrija wa kutolea mkojo nje (urethra) na kufanya mkojo utoke kwa shida.
epididymo- orchitis na kumsababishia ugumba. Kisonono ambayo haikupewa tiba ya kutosha inaweza kumletea madhara kwenye tezi dume (prostate) na anaweza kupata makovu ndani ya mrija wa kutolea mkojo nje (urethra) na kufanya mkojo utoke kwa shida.
Kisonono huweza
kusambaa hadi kwenye mifupa na damu hali ambayo ni hatari kwa maisha. Mtu
mwenye gono anaweza kuambukizwa UKIMWI kwa urahisi zaidi.
Tiba Ya Kisonono
Endapo vipimo
vimeonyesha kuwa una kisonono, wewe na mwenzi wako wote mnatakiwa kutibiwa kwa
kutumia antibiotics na kuacha kujihusisha na masula ya mapenzi hadi hapo tiba
itakapokwisha. Baada ya kumaiza tiba, inashauriwa kujipa mapumziko ya angalau
miezi 3 kuhakikisha kuwa maabukizi yote yamekwisha.Ndugu msomaji,
jisikie huru kuuliza maswali au kutoa maoni uliyo nayo kuhusu mada yetu ya leo,
tutafurahi kuona tumekujibu vizuri.
Endapo unatatizo hili basi wasiliana na Dr. Kamfirimbisi kwa Simu:+255655531702 /+255623450753/ +255766105099
kutumia Link ya Whatsapp hapo chini akupe ushauri ni bure
kutumia Link ya Whatsapp hapo chini akupe ushauri ni bure
Bonyeza Link hii DR.KAMFIRIMBISI ili kuwasiana