Showing posts with label NGILI. Show all posts
Showing posts with label NGILI. Show all posts

Saturday, June 20, 2020

Hernia

Ushauri kwa wenyetatizo la hernia
Ngiri (Hernia) ni uvimbe (eneo lililotuna) kutokana na viungo vya ndani ya mwili kusukuma kuta za misuli inayozunguka au kushikilia viungo hivyo. Hernia hutokea wakati kuna udhaifu au kuna tundu kwenye kuta za misuli inayoshikilia na kuviweka viungo vya tumbo kwenye sehemu yake (peritoneum). Udhaifu huo unaweza kuviruhusu viungo vya ndani kusukuma na kupenyeza, na kujenga eneo lililotuna. Unaweza kuwa na hernia ikiwa unaweza kuhisi namna ya eneo laini lililotuna kwenye maeneo ya tumbo au kinena au kwenye kovu ambalo lilitokana na upasuaji. Eneo hili lililotuna linaweza likapotea ukiminya sehemu hiyo au ukijilaza. Unaweza kupata maumivu kwenye eneo hilo hasa ukikohoa, ukiinama au ikinyanyua kitu kizito.
Hernia ni tatizo linalowasumbua watu wengi katika nchi nyingi duniani. Hernia mara nyingi hutokea kwenye maeneo ya tumbo, lakini huweza pia kutokea kwenye sehemu ya juu ya mapaja, kwenye kitovu, na kwenye maeneo ya kinena. Hernia haihatarishi maisha mara moja, lakini haiwezi kuondoka yenyewe na inaweza kuhitaji kufanyika kwa upasuaji.
Hernia mara nyingi hupewa majina kutokana na sehemu ya mwili inapojitokeza, ingawa mara nyingine majina huweza kutolewa kutokana na sababu nyingine za kuitambulisha. Kila hernia hutibiwa tofauti na nyingine kutokana na sehemu iliyopo na sababu nyingine za kitaalamu. Kuwa na elimu ya kutosha ya kila aina ya hernia itakusaidia kujua namna ya kutoa maamuzi sahihi ya tiba yake.
Aina Za Hernia
1. Inguinal (groin hernia)
Inguinal hernias au groin hernias hutokea pale utumbo au mafuta yanaposukuma na kupenya kwenye misuli ya eneo la kinena. Hii ndiyo aina ya hernia inayowasumbua watu wengi zaidi. Inguinal hernia inaweza kuonekana kwa wanaume na wanawake lakini huwapata zaidi wanaume kwa sababu tayari wana kijitundu kidogo kwenye misuli ya kinena kwa ajili ya kupitisha arteri, veni na mrija wa mbegu vinavyoelekea kwenye korodani. Asilimia 97 ya aina hii ya hernia huonekana kwa wanaume.
Hernia inaweza kuwa juu ya misuli ya tumbo (direct inguinal hernia) au inaweza ikafuata njia ya mrija wa shahawa pale unapoacha eneo la tumbo na kuelekea kwenye korodani (indirect inguinal hernia). Inguianal hernia huanza kama uvimbe mdogo ambao huongezeka na muda. Uvimbe unaoonekana ni utumbo au mafuta yanayosukuma misuli.
Uvimbe huweza kupotea kwa kulala na kurudi mwili ukianza shughuli. Uvimbe huu ukiwa mkubwa sana, huenea kutoka kwenye kinena hadi kwenye korodani zenyewe. Hernia ikiwa kubwa sana huleta matatizo kuiondoa.
2. Umbilical (belly button hernia)
Belly button hernia au umbilical hernia kama inavyoitwa mara nyingine, ni pale utumbo au mafuta yanapopenya kupitia sehemu dhaifu ya misuli iliyopo katikati ya tumbo chini ya kitovu. Sehemu hii ndiyo inayopata udhaifu mara nyingi kwa sababu ndiyo sehemu inayopata minyumbuko zaidi wakati tukifanya shughuli yo yote ya mwili.
Umbilical hernia inaweza kuwa moja kwa moja chini ya kitovu, lakini wakati mwingine inaweza kuwa juu kidogo au chini kidogo ya kitovu. Inaweza kuonekana kama kijikokoto kidogo chini ya ngozi, au ikikua inaweza kuonekana kama kijimpira cha gofu au hata kufikia kimpira cha tenisi kama kikiachwa bila tiba.
Kwa watoto wa kufikia hadi miaka 5, hernia hii kwa kawaida huondoka yenyewe. lakini kwa watu wazima hernia hii haipungui na huwa inazidi kuwa kubwa kila wakati. Wanawake kwa kawaida hupata umbilical hernia wakati wa ujauzito, na hupotea yenyewe baada ya kujifungua. Kwa baadhi ya wanawake, kijishimo hiki katika musuli hubakia baada ya kujifungua. Inashauriwa kuwa wanawake wasubiri kwa miezi 3-6 kuona kama hernia hii itafunga yenyewe.
Kama ilivyo kwa hernia nyingine, dalili za kawaida ni maumivu kwenye kitovu. Kutokana na mafuta au misuli kupita kwenye hernia hii, uvimbe utaonekana chini ya ngozi kwenye eneo hilo. Baada ya muda, kama hernia itakuwa kubwa sana, utumbo unaweza kunaswa kwenye hernia hiyo na kuleta madhara kwenye utumbo, vikiambatana na kichefuchefu, kutapika, na kufunga choo.
Kwa sababu hakuna hernia inayopona yenyewe, upasuaji unahitajika. Njia inayopendekezwa hapa ni open surgery kwa sababu tundu ni dogo.
3. Femoral (below the groin)
4. Epigastric (just below the breast bone)
5. Ventral (above the umbilicus)
6. Incisional (through a prior surgery site)
7. Sports
Namna nyingine za kuelezea Hernia:
1. Recurrent (after a prior hernia repair)
2. Unilateral (one side of the body)
3. Bilateral (both sides of the body)
 Sababu Za Hernia
Ukiondoa hernia inayotokana na upasuaji wa awali, mara nyingi hakuna sababu inayoeleweka ya kusababisha hernia. Watu walio kwenye hatari zaidi ya kupata hernia ni wenye umri mkubwa, na wanaume wapo kwenye hatari zaidi kuliko wanawake.
Hernia inaweza kujitokeza mtoto anapozaliwa au kwa watoto waliozaliwa na dosari kwenye kuta za matumbo yao.
Shughuli au madawa yanayosababisha mgandamizo kwenye kuta za tumbo vinaweza kusababisha hernia. Vitu hivi ni pamoja na:-Kujikamua kwa nguvu wakati wa haja kubwa, kutokana na choo kuwa kigumu,Kikozi cha mara kwa mara,Kuwa na tatizo la cystic fibrosis,Kuvimba kwa tezi dume,Unene wa kupindukia,Kukojoa kwa shida,Kunyanyua vitu vizito,Maji tumboni,Lishe duni uvutaji wa tumbaku,Korodani zisizoshuka,Uchovu wa mwili
 Dalili Za Hernia:-Mara nyingi, hernia ni uvimbe unaoonekana usio na mauvimu na usiohitaji tiba ya haraka. Lakini wakati mwingine, inaweza kukukosesha raha na kuwa na maumivu, dalili zikiongezeka wakati umesimama au wakati unanyanyua vitu vizito. Watu wengi huona uvimbe ukizidi na hatimaye humwona daktari.
Kuna wakati ambapo hernia inahitaji huduma ya haraka ya upasuaji, kwa mfano, pale sehemu ya utumbo inapokuwa imezibwa na hernia ya tumbo (inguinal hernia).
Hatua za haraka za uchunguzi zinatakiwa zichukuliwe wakati inguinal hernia inapoanza kuonyeza dalili kali za:
. Maumivu
. Kusikia kichefuchefu
. Kutapika
Uvimbe wa hernia yenye dalili hizi mara nyingi ni mgumu na huleta maumivu na hauwezi kusukumwa urudi ndai ya tumbo.
Hiatal hernia inaweza kuleta dalili za acid refluc kama kiungulia, kinachotokana na tindikali za tumboni kupanda kwenye koromeo.

Wednesday, May 13, 2020

NGILI

Dr. Kamfirimbisi nimekuja kufundisha somo la ngiri sehemu ya kwanza nitachambua kwa uchache kwa leo twende tuanze somo letu:-
Ngiri hujulikana pia kama “Hernia” kwa Kiingereza. Ugonjwa wa mshipa wa ngiri ni matokeo anayopata mtu kutokana na misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikilia au kubeba viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi na kupelekea viungo hivyo kutoshikiliwa vizuri katika sehemu vinapostahili kuwepo.


Tunaweza kuufahamu zaidi ugonjwa wa ngiri kama hali inayotokea katika mwili ambapo sehemu fulani ya nyama ya viungo mbalimbali vya mwili hujipenyeza kupitia sehemu iliyo dhaifu ya mwili na kutokeza upande wa pili. Sehemu inayoathiriwa mara nyingi ni maeneo ya tumbo, kokwa, korodani na kadhalika ambapo baadhi ya viungo vya mwili vilivyomo tumboni hujipenyeza kupitia vitundu vinavopitisha mishipa ya fahamu inayohudumia kokwa (Spesmatic Cord), hivyo baada ya kujipenyeza huteremka hadi ndani ya korodani hali ambayo hukamilisha kuwepo kwa ugonjwa wa mshipa wa ngiri.

Sehemu ambazo Ngiri inaweza kutokea ni pamoja na maeneo ya:-

a)Tumboni

b)Eneo la kinena

c)Eneo la paja kwa juu

d)Eneo ambalo mtu amewahi kufanyiwa upasuaji siku  za nyuma

e)Kifuani

Ugonjwa huu wa ngiri unawapata watu wa jinsia zote na wa umri wowote

AINA ZA NGIRI

Ugonjwa wa mshipa wa ngiri unaweza kujitokeza maeneo mbalimbali ya mwili na aina ya ngiri hutegemea na sehemu ngiri ilipojitokeza.

NGIRI MAJI

Hii ni aina ya ngiri ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama (hydrocele)

NGIRI KAVU (HERNIA)

Hujulikana pia kama ‘fermoral hernia’ kwa wanawake na huitwa ‘scrotal hernia’ kwa wanaume.

Ngiri ya kwenye kifua Hujulikana pia kitaalamu kama ‘hiatus hernia’

NGIRI YA TUMBO  Hujulikana pia kama ‘Abdominal Hernia’

NGIRI YA KWENYE KITOVU

Hujulikana pia kama ‘Umbilical Hernia”.

NGIRI YA SEHEMU YA HAJA KUBWA

Hujulikana pia kama ‘Anal Hernia’

DALILI ZAKE KWA MWANAUME:

DALILI ZA UGONJWA WA NGIRI

Dalili za ugonjwa huu wa ngiri ziko nyingi sana kwa hiyo hapa nitataja dalili chache tu.

Nazo ndizo hizi zifuatazo:-

1.Kubana tumbo hasa chini ya kitovu wakati wa baridi 

    au unapokula vitu vitamu.

2.Kupiga mingurumo tumboni.

3. Kujaa gesi tumboni.

4. Kuhisi haja kubwa na ukifika chooni unatoa upepo tu.

5. Kupata haja ngumu kama ya mbuzi.

6. Kukaa siku kadhaa bila kwenda haja kubwa.

7. Wakati fulani unakwenda haja sana, kila mara.

8. Unaweza kufanya jimai mara moja tu kisha hamu

     inakuishia hupati nguvu tena mpaka kesho.

9.  Nuru ya macho hupotea taratibu.

10. Hutokea wakati mwingine kufanya jimai mwanzo 
      kabisa au katikati ya tendo gari linazimika.

11. Huvutwa makende au upande mmoja maumivu.

12. Hupiga mishale sehemu za haja kubwa na 
      pembeni karibu na tupu.

13. Maumivu makali ya mgongo au kiuno

14. Uume kusinyaa na kunywea kama wa mtoto

Hizo ni dalili chache endapo ukiwa na dalili moja wapo kati ya hiyo basi ww juwa kuwa una ngiri wasiliana na Dr. kamfirimbisi kupata tiba ya kuondoa tatizo ilo kwa muda mfupi


DR. KAMFIRIMBISI kwa namba :-
+255655531702 /+255766105099
+255623450753
 au tembelea blog yake drkamfirimbisi82.blogspot.com
Endapo unatatizo hili basi wasiliana na Dr. Kamfirimbisi kwa kutumia link ya whatsapp hapa chini

Bonyeza Link DR.KAMFIRIMBISI   
  

Contact Form

Name

Email *

Message *