UFAHAMU UGONJWA WA TETEKUWANGA:
TETEKUWANGA NI NINI?
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi kwa jina la varicella zooster, ugonjwa huu hushambulia mfumo wa hewa wa upumuaji.
Baadae ugonjwa huu hushambulia maini, bandama kisha huenda kwenye ngozi, kwenye ngozi ugonjwa huu huleta upele mwingi mwilini.
Ugonjwa huu hushambulia watoto wenye umri wa miaka mitano mpaka kumi lakini huweza kushambulia umri wowote ule.
Ukishapata ugonjwa huu huwezi kuugua tena lakini ikitokea kinga yako ikashuka sababu ya ugonjwa kama ukimwi, kisukari au mlo mbovu ugonjwa huu hurudi kama mkanda wa jeshi.
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na virusi kwa jina la varicella zooster, ugonjwa huu hushambulia mfumo wa hewa wa upumuaji.
Baadae ugonjwa huu hushambulia maini, bandama kisha huenda kwenye ngozi, kwenye ngozi ugonjwa huu huleta upele mwingi mwilini.
Ugonjwa huu hushambulia watoto wenye umri wa miaka mitano mpaka kumi lakini huweza kushambulia umri wowote ule.
Ukishapata ugonjwa huu huwezi kuugua tena lakini ikitokea kinga yako ikashuka sababu ya ugonjwa kama ukimwi, kisukari au mlo mbovu ugonjwa huu hurudi kama mkanda wa jeshi.
Ugonjwa unaambukizwaje?
Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya hewa au kugusana na mgonjwa na baada ya siku 11 mpaka 20 baada ya kuambukizwa dalili za kwanza za ugonjwa huu hutokea.
Ugonjwa huu huambukizwa kwa njia ya hewa au kugusana na mgonjwa na baada ya siku 11 mpaka 20 baada ya kuambukizwa dalili za kwanza za ugonjwa huu hutokea.
DALILI ZA TETEKUWANGA NI ZIPI?
Mwanzoni kabisa huanza homa, kikohozi na mwili kuchoka baadae ngozi hujaa vipele vikubwa vinavyowasha ambavyo husambaa kwanzia usoni, mikononi, miguuni na tumboni
Mwanzoni kabisa huanza homa, kikohozi na mwili kuchoka baadae ngozi hujaa vipele vikubwa vinavyowasha ambavyo husambaa kwanzia usoni, mikononi, miguuni na tumboni
Jinsi ya kugundua ugonjwa:
vipimo vya maabara sio lazima kwani ugonjwa unaweza kugundulika kwa kuangalia
vipele na kuvitambua kama picha inavyoonyesha.
MATIBABU:
mgonjwa huweza kupona bila dawa yeyote lakini kwa mgonjwa ambaye kinga yake imeshuka anaweza kupewa dawa ya kupunguza makali ya ugonjwa. Baada ya wiki moja mpaka mbili vipele huanza hukauka kabisa na kwa kutoa maji na kuacha makovu.
mgonjwa huweza kupona bila dawa yeyote lakini kwa mgonjwa ambaye kinga yake imeshuka anaweza kupewa dawa ya kupunguza makali ya ugonjwa. Baada ya wiki moja mpaka mbili vipele huanza hukauka kabisa na kwa kutoa maji na kuacha makovu.
MADHARA YA KUUGUA UGONJWA HUU:
Ugonjwa huu huweza kusababisha matatizo ya moyo,figo, ini, kifua, jointi za miguu na mikono, na matatizo ya mishipa ya fahamu.
Jinsi ya kuzuia ugonjwa huu:
Mgonjwa anatakiwa atengwe mbali na watu wengine huku nguo zake na mashuka yake yakifuliwa kwa makini sana kwa kutumia gloves ili kutoambukiza watu wengine.
Ugonjwa huu huweza kusababisha matatizo ya moyo,figo, ini, kifua, jointi za miguu na mikono, na matatizo ya mishipa ya fahamu.
Jinsi ya kuzuia ugonjwa huu:
Mgonjwa anatakiwa atengwe mbali na watu wengine huku nguo zake na mashuka yake yakifuliwa kwa makini sana kwa kutumia gloves ili kutoambukiza watu wengine.