Tuesday, June 2, 2020

FAIDA YA MZEITUNI

Faida ya  Tunda la Mzeituni

  1. Ni tiba nzuri sana ya  vidonda ,mabaka na makovu ya mwilini
  2. Yanaweza kutumika kwa kulainisha ngozi
  3. Yanasaidia kutibu tatizo la mzio wa ngozi
  4. Yana kiasi kikubwa cha Vitamin A,D,E na K ambazo zinamsaidia kuondoa sumu ya kwenye ngozi
  5. Matumizi ya mafuta ya mzeituni yataifanya ngozi yako iendelee kuonekana changa na yenye afya wakati wote
  6. Matumizi ya mafuta ya mzeituni yanasaidia kutibu matatizo na magonjwa yote ya ngozi
  7. Vilevile matumizi ya mafuta ya mzeituni kama chakula yanasaidia kuimarisha na kurutubisha afya ya mtumiaji.
  8. Matumizi ya mafuta ya mzeituni kama chakula yanasaidia kupunguza uzito kwa watu wenye matatizo ya uzito mkubwa.
Mafuta ya zaituni yana manufaa mengi katika mwili na maisha ya binadamu kwa ujumla kama ifuatavyo:-

  • Mafuta ya zaituni hutibu maumivu ya tumbo kwa kunywa kijiko 1 mara 2 kwa siku kwa muda wa siku 7 hadi siku 11 Inshaallah utapona kabaisa
  • Mafuta ya zaituni hutibu masheitani kwa kusomea kisomo cha Ruqia , mgonjwa atajipaka mwili mzima mara moja kwa siku pamoja na kutafuta vitunguu saumu punje tatu wakati wa kulala kwa muda wa siku arobaini. Inshaallah
  • Mafuta ya zaituni ni kinga ya masheitani wa kijini na wa kibinadamu kwa kujipaka mwili mzima mara moja kwa siku
  • Mafuta ya zaituni hutibu ugonjwa wa mafua kwa kupaka kwenye mwamba wa pua na ndani ya matundu ya pua mara tatu kwa siku
  • Tiba ya vidonda vya tumbo, Matumizi ni kutia vijiko 2 vya chakula katika uji mara mbilui kwa siku kwa muda wa siku 90
  • Mafuta ya zaituni hutumika kama huduma ya kwanza kwa aliyekunywa sumu kwa  kunywa na kwa mwenye ganzi au kiharusi hutumia kwa kuchua mwili asubuhi na jioni
  • Mafuta ya zaituni hutumika katika kuua wadudu wabaya walioko tumboni kwa njia ya kunywa kijiko kimoja mara mbili kwa siku kwa muda wa siku saba
  • Mafuta ya zaituni huongeza nguvu za kiume kwa kunywa kujiko kimoja kwa siku pamoja na kuuchua uume mafuta yaliyochanganywa na vitunguu swaumu kwa muda wa siku saba hadi kumi na moja
  • Tiba ya ugonjwa wa kusahau, pakla katika paji la uso kutwa mara mbili pamoja na kunywa kujiko kimoja cha chai mara moja kwa siku  kwa muda siku 7 hadi siku 11
  • Tiba ya degedege, hutumika kupakaa mwili mzima mafuta yaliosomewa Ruqya mara mbili kwa siku kwa muda wa siku 7 hadi siku 21
  • Kukojoa kitandani, kupkaa mafuta ya zaitun mwili mzima kutwa mara mbili huku akilamba matone mawili kwa muda wa siku 7 hadi siku 21

Contact Form

Name

Email *

Message *